• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Vyama vya Akiba, Mikopo Zanzibar Vyajifunza Wilayani Njombe

Tarehe iliyowekwa: November 15th, 2017

Wadau wa vyama vya akiba na Mikopo, vyama vya kilimo na masoko kutoka Zanzibar wakiongozwa na wataalamu kutoka katika Wizara ya kazi, uwezeshaji, wazee, vijana, wanawake na watoto Zanzibar wamefanya ziara ya kujifunza namna vyama hivyo vinavyofanya kazi  katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Katika ziara hiyo ambayo imefadhiliwa na Programu ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF), walipata nafasi ya kutembelea  vyama vya kilimo na masoko (AMCOS) na akiba na Mikopo (SACCOS) vya  Ibumila pamoja na Ninga zilizopo wilayani Njombe.

Wakiwa wilayani hapa wamejifunza namna mfumo wa stakabadhi gharani unavyoendeshwa , SACCOS zilivyojikita  katika utoaji wa  huduma za kifedha, utoaji wa mikopo na urejeshaji wake,  namna AMCOS zilivyojikita katika kukusanya mazao na kuwatafutia masoko wanachama wake pamoja na ushirikiano uliopo  baina ya vyama vya akiba na mikopo pamoja na serikali za vijiji.

Akizungumzia namna Halmashauri ya wilaya ya Njombe inavyozisaidia SACCOS na AMCOS,  Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo, Monica Kwiluhya alisema kuwa Halmashauri imekuwa ikipitishia fedha za kuwezesha vikundi vya  vijana na wanawake katika SACCOS jambo ambalo linaziongezea Saccos  wanachama  pamoja na kurahisisha ufuatiliaji upande wa  Halmashauri kwa kuwa fedha hizo hufuatiliwa Saccos na sio kwa wanavikundi.

Aliongeza kuwa Mwaka huu Halmashauri imeziwezesha AMCOS kwa kuwaunganisha wanachama wake na benki ya kilimo kwa ajili ya kupata pembejeo za kilimo pamoja na  kupima mashamba yote ya wanachama wa AMCOS ili kuwawezesha kupata hatimiliki za kimila zitakazowawezesha kupata mikopo kwenye taasisi za kifedha kwa ajili kilimo.

“Tumepima mashamba yote ya wanachama wa AMCOS ijapokuwa ni gharama lakini kwa kuthamini umuhimu wao tumepima kwa nusu gharama ambapo fedha zinazobaki watalipa baada ya mavuno” alisema Kwiluhya.

“ Wakati wa maonyesho ya nane nane huwa tunawachukua wanachama na kuwapeleka Mbeya kwa ajili ya kuwatafutia masoko ambapo mwaka huu tumefanikiwa kuwaunganisha na wafanyabiashara kutoka katika nchi ya Botswana kwa ajili ya soko la asali” aliongeza Kwiluhya

Alifafanua kuwa  AMCOS za Halmashauri ya wilaya ya Njombe zinasaidiwa kwa kutafutiwa miradi ya kuongeza thamani na kuitaja AMCOS ya Ninga kama mfano ambayo iko hatua ya mwisho kununua mashine kwa ajili ya kusaga unga na kuuza badala ya kuuza mahindi.

“Halmashauri kwa kushirikiana na mradi wa MIVARF tumejenga kiwanda kidogo cha mafunzo kwa vikundi vya wakulima kuzuia upotevu na kuongeza thamani ya mazao na  kiwanda hiki kitaanza kufanya kazi mwezi Januari ” alisema Kwiluhya.

Kwa upande wake Ally Mohamed Ally ambaye ni afisa ushirika Pembe alisema kuwa wamepata uzoefu mkubwa ambao watakwenda kuutumia kuboresha utendaji kazi wa SACCOS na AMCOS Unguja na Pemba.

“Tumejifunza namna mikopo inavyotolewa, nguvu ya Halmashauri kwenye SACCOS, uhamasishaji unavyofanyika pamoja na namna SACCOS na AMCOS zinavyoshirikiana. Hakika safari yetu imekuwa ya mafanikio makubwa na tutakwenda kutekeleza kama tulivyojifunza” alisema Ally.

Nae mkuu wa wilaya ya Njombe Bi Ruth Msafiri akizungunza na ugeni huu ulipomtembelea ofisini kwake aliwataka kuyafanyia kazi yote waliyojifunza na kuacha kuchanganya siasa na masuala ya utendaji kazi.

“ Naomba mkawe waangalifu mkikosea kwenye kuchagua viongozi wazuri wa Saccos na Amcos hamtaweza kusonga mbele, mkioneana aibu na kuchangua viongozi wabovu watakuwa chanzo cha uharibifu, wizi wa mali za wanachama pamoja na kupunguza uaminifu jambo litakalochelewesha maendeleo” alisema Msafiri.

Halmashauri ya wilaya ya Njombe inajumla ya vyama vya ushirika 34, vyama vya akiba na mikopo 12 vyama vya kilimo na masoko 18. Vyama vya wafugaji vitatu, na chama cha Muungano kimoja.  Hadi sasa Vyama hivyo vinamtaji wa Bilioni 3.34 huku mikopo yenye thamani ya bilioni 17.9 ikiwa imeshatolewa.

Vyama vya ushirika wilani Njombe vinajumla ya wananchama 8,384 ambapo wanaume ni 4,471 na wanawake 3153 huku kukiwa na vikundi 638 na taasisi 122.

Katika siku za hivi karibuni Halmashauri ya wilaya ya Njombe imekuwa ikitembelewa na Halmashauri mbalimbali nchini ambazo zimekuwa zikijifunza masuala mbalimbali ikiwemo kampeni ya afya na usafi wa mazingira ambapo Halmashauri ilishika nafasi ya kwanza upande wa vijiji Tanzania bara.

Tayari Halmashauri za mkoa wa Geita, Dodoma pamoja na Manispaa ya Singida zimefanya ziara ya mafunzo katika Halmashauri ya wilaya ya Njombe.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa