• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Uchefuaji- Mbinu shirikishi jamii iliyoleta mafanikio kampeni ya afya na Usafi wa mazingira Njombe

Tarehe iliyowekwa: September 19th, 2018

Katikati ya mkutano mkuu wa Kijiji , wataalamu kutoka Halmashauri ya wilaya ya Njombe wanasimama na kuanza kutoa vifurushi walivyokuwa navyo.

Kila mmoja kwenye mkutano anaangalia kwa makini ni kitu gani hasa kinatolewa na hakuna ambaye anabaini mapema.

Mara kutoka kwenye moja ya vile vifurushi kinatolewa kinyesi cha binadamu mbele ya kadamnasi.

Ndio! kinyesi cha binadamu tena ambacho hakijakauka. Wananchi wanapigwa na butwaa ,wanaanza kuona kinyaa na kulalamika. Kisha mtaalam kutoka Halmashauri anawaambia wananchi kwanini wanaona kinyaa wakati kila siku wanakula kinyeshi ndio maana magonjwa ya kuhara na tumbo hayaishi miongoni mwao.

Anawaeleza kinaga ubaga kuwa kinyeshi hicho wamekitoa mita chache tu kutoka katika maeneo wanayokaa na kimetapakaa karibu kila kona.

Ni kweli kulingana na mazingira ya Njombe na mwamko mkubwa wa wananchi katika upandaji wa miti , sehemu kubwa ni misitu au mazao hivyo ni lahisi kwa wananchi kujisaidia ovyo.

Mbinu hii inaitwa Uchefuaji yaani mbinu shirikishi jamii (CLTS).

Mbinu hii ilitumika kuihamasisha jamii kuanzia ngazi ya vitongoji. Ni mbinu inayotia kinyaaa lakini yenye kuleta mafanikio.

Ili kuweza kufanikisha kampeni ya afya na usafi wa mazingira katika Halmashaur ya wilaya ya Njombe  jambo la kwanza walilofanya wataalam kutoka Halmashauri ilikuwa ni kutoa elimu kwa viongozi wa ngazi za vitongoji. Kisha wakaambatana nao kusaka vinyesi na kwenda kuwachefua wananchi kwenye mkutano wa hadhara.

Baada ya kupata elimu kupitia  mbinu shirikishi jamii ya uchefuaji wananchi walihamasika na kuacha kujisaidia ovyo na kujenga vyoo bora, miundombinu ya kunawia mikono kwa maji tiririka pamoja na kuvitumia vyoo hivyo.

Mbali na kuhamasika ziliundwa kamati za usimamizi wa utekelezaji kampeni ya afya na usafi wa mazingira ngazi ya Kitongoji, kijiji na Kata. Kazi kubwa ya kamati hizi ilikuwa kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara.

Sambamba na hilo timu ya ufuatiliaji kutoka Halmashauri ya wilaya ya Njombe haikuwa nyuma katika kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na kufanya vikao na kamati za vitongoji, vijiji na Kata ili kushirikiana kutatua changamoto wazazokutana nazo katika utekelezaji wa Kampeni.

Sasa vijiji vya Sovi na Image vina kaya zenye vyoo bora kwa asilimia 100 na miundombinu ya kunawia mikono. Ndio ni kijijini lakini kuna vyoo vya sinki kama mjini.

Mazingira ya vijiji hivi kwa sasa ni safi na hakuna vinyesi vilivyotapakaa mitaani, mashambani pamoja na kwenye vichaka.

Ama kwa hakika uchefuaji kiboko!.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa