• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Zaidi ya wasichana 1062 kupewa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi Njombe

Tarehe iliyowekwa: April 25th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imezindua chanjo kwa ajili ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi ambapo zaidi ya wasichana 1,062 wanatarajiwa kupewa chanjo wilayani hapa.

Chanjo hiyo ambayo inatolewa bure kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 itatolewa katika vituo vyote vya kutolea huduma za afya vilivyopo katika maeneo mbalimbali ya Kata na vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Akisoma taarifa kuhusu chanjo wakati wa uzinduzi ulifanyika katika kijiji cha Nyombo Kata ya Ikuna wilayani Njombe, Mkurugenzi mtendaji wa Halamshauri ya wilaya ya Njombe, Monica Kwiluhya alisema kuwa , wamejipanga kikamilifu katika zoezi hilo kwa kufikia zaidi ya asilimia 95 ya walengwa.

Bi kwiluhya alibainisha kwamba  tayari chanjo imesambazwa katika vituo vya kutolea huduma za afya  pamoja na kuandaa orodha ya walengwa wote wanaotarajia kupata chanjo hiyo kwa mwaka 2018 ambapo wengi wao wapo katika shule za Msingi na Sekondari.

“Tumeshaandaa  vituo vitakavyotoa huduma hizi kwa njia ya mkoba (outreach services) katika vijiji vyote vya Halmashauri  pamoja na kutoa mafunzo ya utoaji wa chanjo  kwa walimu wa shule za msingi na sekondari kutoka shule zote zilizopo katika Halmashauri” alisema Bi Kwiluhya.

Alieleza kuwa elimu na maelekezo juu ya chanjo ya kuziua saratani ya mlango wa kizazi imetolewa kwa  wakuu wa idara na vitengo vya Halmashauri pamoja na kufanya uhamasishaji  kwa jamii ili wananchi waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo kupitia vyombo mbalimbali vya habari vinavyopatikana katika Halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Chanjo hii itasaidia kikamilifu jitihada za kupambana na ugonjwa wa saratani ambao umekuwa ni chanzo kikubwa cha vifo vya akinamama wengi nchini. Tafiti zinaonesha kuwa saratani ya mlango wa kizazi pamoja na saratani ya matiti huchangia zaidi ya asilimia 50% ya vifo vyote vinavyosababishwa na saratani nchini.

Chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi itatolewa kwa dozi mbili kwa kila mlengwa wa chanjo ambapo mara ya kwanza itatolewa msichana anapofikisha miaka 14 na dozi ya pili itatolewa baada ya miezi 6 tangu kutolewa kwa dozi ya kwanza.

Aidha, imebainishwa  na wataalamu wa masuala ya afya kuwa lazima mtu akamilishe dozi zote mbili kwa kuwa mtu akikosa dozi moja anakuwa ajakingwa

Uzinduzi wa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi kitaifa ulifanywa na Makamu wa Rais, Samia  Suluhu Hassan, jijini Daresalaam Aprili 10 mwaka 2018.





Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa