• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Waratibu Elimu Kata wapewa Pikipiki Njombe

Tarehe iliyowekwa: July 27th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imepokea msaada wa pikipiki 12 kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI)  kupitia mradi wa kukuza stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu ili kuboresha maendeleo ya elimu wilayani Njombe.

Pikipiki zilizotolewa ni aina ya   Honda  ambazo zimegharimu  milioni 36 na  zitatumiwa na waratibu elimu Kata katika kufuatilia maendeleo ya elimu  kwenye shule za msingi  53 na Sekondari  14 zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Akizungumza  wakati wa makabidhiano ya pikipiki hizo mbele ya viongozi wa ngazi ya Mkoa na wilaya,  Bw  Salum Mkuya kutoka idara ya Uratibu na Usimamizi wa Elimu TAMISEMI alisema kuwa pikipiki hizo zimeletwa ikiwa ni jitihada za serikali katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

“Rais anadhamira ya dhati katika kuboresha elimu nchini  alianza na elimumsingi bila malipo na juzi ameleta vitabu kwa ajili ya darasa la nne na sasa pikipiki kwa ajili ya kusimamia masuala ya elimu” alisema Mkuya

Bw Mkuya aliwataka waratibu kufanya kazi kwa juhudi na maarifa huku wakizingatia maadili ili kuongeza kiwango cha ufaulu katika wilaya ya Njombe kwa kuwa tayari nyenzo muhimu itakayowawezesha kusafiri maeneo mbalimbali kwa ajili ya ufuatiliaji wa elimu wanayo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Njombe , Ruth Msafiri aliwataka Waratibu Elimu Kata kutumia pikipiki hizo kwa kazi iliyokusudiwa huku akiagiza wale wote watakaotumia kinyume na madhumuni kuchukuliwa hatua za kisheria.

“Ile dhana ya kuwa mali za serikali hazina mwenyewe muifute kabisa naomba mkavitunze vyombo hivi na mvitumie vizuri, msivigeuze kuwa bodaboda au vyombo vya kuendea shambani badala ya kufuatilia masuala ya elimu  na mviendeshe kama watumishi wa umma” alisema Msafiri.

“Tunaishukuru serikali kwa kutuletea pikipiki hizi kwa ajili ya waratibu elimu Kata, tuliweza kufanya vizuri bila kuwa na nyenzo sasa tumepata nyenzo tutahakikisha ufaulu unakuwa kwa asilimia 100.”Aliongeza  Msafiri.

Aliongeza kuwa uwepo wa vitendea kazi  utaamsha na kuongeza hali ya uwajibikaji na maendeleo ya elimu katika Halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Alibainisha kuwa wilaya ya Njombe imeweka utaratibu wa kufanya vikao mara mbili kwa mwaka vikiwa na lengo la kufanya tathimini ya masuala ya elimu pamoja na kufanya ziara za mara kwa mara kwenye Shule kufanya kaguzi mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba ya waratibu elimu Kata wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe  baada ya kupewa pikipiki Bw. Neno Lulandala ambaye ni mratibu elimu Kata ya Kichiwa aliahidi kutumia vyombo hivyo kufuatilia maendeleo ya elimu ili kuinua kiwango cha ufaulu kwenye shule.

“Kwanza tunaishukuru serikali kwa kutupatia vyombo hivi ambavyo vitarahisisha sana ufuatiliaji wa masuala ya elimu kwenye shule za Sekondari na Msingi, kwa niaba ya wenzangu tunaahidi kutumia pikipiki hizi kwa madhumuni yaliyokusudiwa ili kuinua kiwango cha taaluma katika wilaya yetu” alisema Lulandala.

Halmashauri ya wilaya ya Njombe inajumla ya Kata 12 ambapo kila Kata ina mratibu elimu wake. Upande wa shule za Sekondari ziko 14 huku shule za serikali zikiwa 11 na binafsi zikiwa tatu. Upande wa shule za Msingi Halmashauri ya wilaya ya Njombe shule 53,  shule za serikali zikiwa 52 na binafsi ikiwa moja.


Mwakilishi kutoka Idara ya Uratibu na Usimamizi wa Elimu ya TAMISEMI ,Salum Mkuya (watatu kutoka kushoto) akimkabidhi mkuu wa Wilaya ya Njombe Ruth Msafiri funguo za pikipiki kwa ajili ya waratibu elimu Kata wa Halmashauri ya willaya ya Njombe


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe , Frank Komba akimkabidhi Neno Lulandala mmoja ya waratibu elimu Kata funguo za Pikipiki zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya waratibu elimu Kata wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa