• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Wanaowapa mimba watoto kushughulikiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama Njombe.

Tarehe iliyowekwa: July 5th, 2017

Kamati ya Ulinzi na usalama ya wilaya ya Njombe imejipanga kuwashughulikia na kuwathibiti wote ambao wanawapatia mimba watoto kama wanavyoshughulikiwa wezi wilayani hapa 

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Bi Ruth Msafiri wakati akifungua kikao cha kufanya tathimini juu ya ukatili dhidi ya watoto kwa wadau mbalimbali Wilayani hapa wakiwemo madiwani, wakuu wa Idara na Vitengo, wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali ,vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na timu ya Ulinzi na usalama wa mtoto ya Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Akizungumza katika kikao hicho Bi Msafiri alisema kuwa jamii inapaswa kushiriki katika kuwalinda watoto wa kike ili waweze kutimiza ndoto zao kwa kuwa watoto wa leo ni viongozi wa kesho. Aliongeza kuwa suala la kuwalinda watoto lazima yafanyike maamuzi magumu ambayo yatakuwa mfano kwa wale wote wenye tabia ya kufanya ukatili dhidi ya watoto.

Alisema kuwa wazazi na jamii lazima wajenge mazoea ya kukaa na watoto wa kike na kiume na kuwafundisha elimu ya kujitambua pamoja na wazazi kuhakikisha wanatoa taarifa na kuwafichua wanaofanya ukatili dhidi ya watoto katika maeneo yao.

“ Elimu kwa watoto wetu ni muhimu na vianzishwe kwa wingi vikundi vya TUSEME katika shule zetu ili vitumike katika kutoa elimu shuleni, tutapata taifa lisilokuwa na maendeleo endapo tutaruhusu watoto wapewe mimba” alisema Bi Msafiri.

Aliongeza kuwa endapo mtoto atapewa mimba wazazi watawajibika kutoa maelezo juu ya swala hilo huku akitaja kifo kuwa ni miongoni mwa athali za mimba za utotoni kwa watoto kutoka na via vya uzazi kutokomaa

Aliwataka wazazi kuhakikisha wanaendelea kuchangia chakula cha mchana kwenye Shule pamoja na kuwapatia lishe bora ikiwemo kuzingatia ushauri wa madaktari katika suala la unyonyeshaji wa watoto ili kupunguza hali ya udumavu kwa watoto.

Sambamba na hilo Bi Msafiri aliwataka madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kuhakikisha wanapopitisha bajeti suala la ulinzi na usalama wa watoto linapewa kipaumbele ili kuweza kutokomeza vitendo vya ukatili .

“Mtoto wa leo ni kiongozi wa kesho na mustakabali wa taifa letu hapo baadae hivyo hakikisheni bajeti ya wilaya inatenga fungu la kutosha linalolenga kuhudumia watoto katika Nyanja zote za makuzi ya mtoto ikiwemo chekechea na awali, mifumo ya ulinzi ngazi zote za Vijiji na Kata pamoja na ulinzi wa Kisheria.” Aliongeza Bi Msafiri.

Aidha, alipiga marufuku msemo wa mtoto wa mwenzio ni mkubwa mwenzio na kuahidi kuwachulia hatua wale wato wanaokwenda kinyume na maagizo ya Rais ikiwemo wanaopinga walipewa mimba kutoendelea na shule kama ilivyoagizwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli.

Hadi sasa Wilaya ya Njombe inajumla ya matukio 43 ya ukatili wa watoto ikiwemo matukio 26 ya ubakaji. Katika matukio hayo mashauri yaliyoisha yako tisa huku mashauri manne washitakiwa wamepewa adhabu ya kifungo na mashauri matano washitakiwa wameachiwa huru baada ya kukosekana kwa ushahidi na mashaidi.

Aidha, mashauri tisa yako katika hatua ya usikilizwaji, mashauri manne yako hatua ya kusoma hoja na mashauri 18 yapo katika hatua za kutajwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa