• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Shule ya Msingi Image Kielelezo cha Mafanikio ya Kampeni ya afya na Usafi wa Mazingira Njombe

Tarehe iliyowekwa: July 30th, 2018

Unapofika katika kijiji cha Image ambacho ni miongoni mwa vijiji vya mfano Tanzania katika utekelezaji wa kampeni ya afya na usafi wa mazingira, moja ya kivutio kikubwa ambacho ni kielelezo tosha cha mafanikio ya Kampeni ya Afya na usafi wa wa mazingira ni utunzaji wa mazingira katika shule ya Msingi Image iliyopo katika kijiji cha Image Kata ya Kidegembye katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Mbali na kuwepo na ndoo za kuzolea uchafu karibu kila baada ya mita kadhaa, shule hii imezungukwa na mabango yenye ujumbe wa aina mbalimbali unaosisitiza elimu na usafi wa mazingira.

Shule ya Msingi Image ambayo ilianzishwa mwaka 1974 mbali ya kuwa na vyoo bora vilivyozingatia mahitaji maalum  kwa walemavu na wasichana waliopevuka, inamiundombinu ya kunawia mikono baada ya kutoka chooni.

Miundombinu hii imewafanya wanafunzi kutougua magonjwa yatokanayo na uchafu ambapo hapo awali kabla ya Kampeni ya afya na usafi wa mazingira idadi kubwa ya wanafunzi walikuwa wakikabiliwa nayo.

Shule hii ni miongoni mwa shule za msingi zinazotekeleza kampeni ya afya na usafi wa mazingira kupitia shirika la UNICEF pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Kupitia kampeni ya afya na usafi wa mazingira, kiwango cha ufaulu kimeongezeka kutokana na kuwepo kwa mazingira rafiki ya kujifunzia na kufundishia.

Kwa mujibu wa mkuu wa shule ya Image, Shadrack Sodike alisema kuwa ya  kabla ya kampeni ya afya na usafi wa mazingira kiwango cha ufaulu kilikuwa kidogo kuliko sasa.

Alisema kuwa  kampeni ya usafi wa mazingira imewezesha ujenzi wa vyoo bora jambo ambalo limechochea wanafunzi wengi kufika shuleni hususani wasichana kutokana na kutokuogopa na kuwepo na mazingira mazuri ya kuwasitiri wawapo katika hedhi hivyo kupata muda wa kusoma zaidi wa kujifunza tofauti na ilivyokuwa hapo awali.

"Awali wanafunzi wa kike waliopevuka kila mwezi walikuwa wanakosa masomo wakati mwingine hadi wiki moja jambo lililochangia kuathili maendeleo yao kitaaluma, hii ilitokana na miundombinu kutokuwa rafiki hivyo kulazimika kushinda nyumbani, Sasa hakuna mwanafunzi wa kike anayekosa masomo kutokana na vyoo bora vilivyozingatia mahitaji yao ya kibaiolojia" anabainisha Sodike

"Kiwango cha ufaulu kimeongeza ambapo toka mwaka 2014 hatujawahi kushuka chini ya asilimia 80 huku mwaka 2015 na 2016 ufaulu ukiwa kwa asilimia 100" alibainisha Sodike

"Hapa tuna programu ya usafi wa mazingira shuleni (SWASH) wanafunzi wana kikundi chao ambacho kazi yake ni kutoa elimu kuhusu afya na usafi wa mazingira kwa wanafunzi wenzao kwa njia mbalimbali za nyimbo, ngojera na maigizo" aliongeza  Sodike.

Unapokwenda kwenye vyoo vya shule hii ambavyo ni vya sinki huku sakafu yake ni marumaru unakutana na bango lenye ujumbe unaomkumbusha mwanafunzi nini anatakiwa kufanya kabla na baada ya kutoka chooni.

Kwa kuwa wanafunzi wanakula chakula cha mchana shuleni, kimetengwa chumba maalumu kwa ajili ya kuhifadhi maji safi na salama ili kulinda afya za wanafunzi.

Kampeni ya afya na usafi wa mazingira imeleta manufaa makubwa kwa wanafunzi wa Image.


Wanafunzi wa shule ya Msingi Image iliyopo wilayani Njombe wakiimba kabla ya kunawa mikono kwa ajili ya chakula cha mchana, Mbinu hii huwa wanaitumia ili kukumbushana umuhimu wa kunawa mikono kabla na baada ya kula pia wakati wa kutoka chooni.


Moja ya mabango yaliyo na ujumbe unaomkumbusha mwanafunzi vitu anavyotakiwa kuvifanya wakati akiingia chooni na baada ya kutoka choo katika shule ya Msingi Image iliyopo wilayani Njombe

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa