• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Naibu Waziri apongeza huduma za Afya Njombe

Tarehe iliyowekwa: July 20th, 2017

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dr Hamis Kigwangalla, ameipongeza  Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa kuboresha huduma katika kituo cha afya Lupembe baada ya  kukarabati chumba cha upasuaji na jengo la mama na mtoto.

Pongezi hizo zimetolewa wakati wa ziara yake aliyoifanya katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe   ambapo alikagua kituo cha Afya Lupembe na Kichiwa ambapo katika kituo cha Afya Lupembe huduma ya upasuaji inatarajiwa kuanza muda wowote.

Akizungumza na wananchi katika Kata ya Lupembe na Kichiwa  mara baada ya kuweka jiwe la Msingi katika jengo la mama na mtoto katika kituo cha afya Lupembe, Dr .Kigwangalla alisema kuwa  ameridhishwa na namna  Halmashauri inavyotekeleza maagizo ya Serikali ikiwemo agizo la kila kituo cha Afya kuanzisha huduma za upasuaji agizo lililotolewa wilayani Meatu.

"Mimi ni mgumu sana kutoa pongezi na kwenye ziara zangu huwa sicheki, siwezi kucheka wakati wakinamama na watoto wanakufa, lakini panapofanyika mambo mazuri lazima tupongeze, hongereni sana kwa kuboresha huduma katika kituo cha afya Lupembe hasa chumba cha upasuaji, hongereni sana ." alisema Dr Kigwagalla.

"Huduma zinazotolewa hapa  ni za kiwango cha hospitali ya Wilaya au Mkoa msione majengo yaliyo mkadharau ,kitaalamu tunaangalia huduma zinazotolewa . Uboreshaji huu utasaidia  kupunguza vifo vya akinamama na watoto kutokana na  kupunguza umbali wa kupata huduma za upasuaji maana nasikia zamani mlikuwa mnakwenda Hospitali ya Mkoa Kibena ambapo ni zaidi ya kilometa 60, sasa huduma zitapatikana hapa hapa" aliongeza Dr Kigwagalla.

Dr kigwangalla alieleza kuwa serikali imeongeza mgao wa dawa na kuitaka  Halmashauri kuhakikisha inasimamia vizuri dawa zote zinazoletwa na kuwachukulia hatua wale wenye kukiuka maagizo ya Serikali.

Akijibu ombi la wananchi wa Kichiwa la kupatiwa gari la wagonjwa kwa ajili ya kituo cha afya, Dr kigwagala alisema kuwa suala hilo atalifanyia  kazi na pindi fursa itakapopatikana Halmashauri ya wilaya ya Njombe itapewa kipaumbele.

Kwa upande wake  Mbunge wa Jimbo la Lupembe lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bw. Joram Isamil Hongoli aliiomba Serikali kupitia  Naibu Waziri, Dr Kigwangalla kusaidia upatikanaji wa mashine za X-ray , Utra Sound pamoja na vifaa vingine muhimu katika vituo vya afya vya Halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe  imeendelea kutekeleza sera ya kuwa na kituo cha afya katika kila  Kata  na  zahanati katika kila kijiji kwa kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo wa ndani na nje ya nchi pamoja na kuwahamasisha wananchi kuanza ujenzi wa vituo vya huduma  katika maeneo ambayo hayana.

Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imetenga shilingi 276,420,522 kupitia vyanzo vya mapato ya ndani na ruzuku kutoka serikali kuu kwa ajili ya kukamilisha maboma matano ya zahanati na kuanza ujenzi wa majengo ya upasuaji katika vituo vya afya vya Mtwango na Kichiwa ambapo vimetengewa  shilingi milioni 70  pamoja na kuanza kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa