• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Mradi wa Umwagiliaji kuwanufaisha Wakulima Njombe.

Tarehe iliyowekwa: October 29th, 2017


Katika kuhakikisha mradi wa umwagiliaji katika kijiji cha Itipingi unatumika kama ilivyotarajiwa na kutoa matokeo chanya kwa wakulima , Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imetoa elimu juu ya matumizi bora ya mradi huo wilayani hapa.

Mradi huu ambao ni miongoni mwa miradi mikubwa ya umwagiliaji Wilayani Njombe ,hadi kukamilika kwake umegharimu zaidi ya Milioni 300 ukiwa na mfereji wa umwagiliaji wenye urefu wa mita 1725 na utawahudumia zaidi ya wakulima 1500 kutoka katika kijiji cha itipingi pamoja na maeneo ya jirani.

Mradi huu unaeneo la umwagilia la hekari 160 ambapo hadi sasa hekari zaidi ya 80 zinatumika na hekari 40 tayari zimelimwa na kupandwa mazao mbalimbali ikiwemo mboga mboga ambazo zinawahakikishia wakulima na wananchi kipato pamoja na chakula bora.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara baina ya wataalamu wa Halmashauri pamoja na wanakijiji cha Itipingi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe , Monica  Kwiluhya alisema kuwa  baada ya kukamilika kwa mradi huo anatarajia kilimo cha kisasa kiendeshwe pamoja na kuulinda mradi ili uweze kutoa manufaa kwa kipindi kirefu.

Alisema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe baada ya kukabidhiwa mradi huo imejipanga kuhakikisha mradi unatumika kadiri ulivyopangwa na kutoa manufaa kwa wakazi wa kijiji cha Itipingi.

“ Leo nimekuja na wataalaumu wote ili waweze kutoa ufafanuzi wa namna mradi huu unavyotakiwa kutumika ili uweze kudumu na mpate mazao bora, pamoja na kulinda maji ili yaendelee kuwepo kwa vizazi  vya leo” alisema Kwiluhya.

Aliwataka vijana kujiunga katika  vikundi na kuomba mikopo kwenye Halmashauri kwa ajili ya kuendesha kilimo hali itakayowawezesha kupata kipato na kujikwamua kiuchumi.

Kupitia mkutano huu wananchi walielezwa namna bora ya utunzaji wa vyanzo vya maji ikiwemo kupanda miti rafiki ya maji, kutokulima kwenye vyanzo vya maji pamoja na kutokupeleka mifugo kwenye vyanzo vya maji na kupitisha mifugo yao kwenye mfereji jambo ambalo litapelekea migogoro baina ya wakulima na wafugaji.

“Ili kuondoa migogoro baina ya wakulima na wafugaji , Nimekuja na wataalamu wa mifugo kwa ajili ya kaangalia eneo la kujenga mabirika ya kunyweshea mifugo ili kuepusha mifugo kuingia kwenye mashamba ya wakulima” alisema Kwiluhya.

Katika mkutano huo wananchi walifundishwa namna ya kuweka akiba ili kuweza kukarabati mradi pindi unapoharibika pamoja na kanuni za kilimo bora ili kuwawezesha kupata mazao mengi yaliyo bora.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa