• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Mradi wa Maji wenye Thamani zaidi ya Milioni 230 wawekewa jiwe la Msingi Njombe

Tarehe iliyowekwa: August 24th, 2017

Naibu Waziri wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe, ameweka jiwe la Msingi katika mradi wa maji Kijiji cha Iwafi kilichopo katika  Halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Uwekaji huo wa jiwe la msingi umefanywa na naibu waziri Kamwelwe wakati akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maji inayotekelezwa katika Halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Mradi huo maji kijiji cha Iwafi  ambao umewekewa jiwe la msingi  hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya Milioni 230 na utahudumia vitongoji sita kati ya vitongoji tisa vilivyopo katika kijiji cha Iwafi Kata ya Idamba. Sambamba na kuhudumia vijiji hivyo mradi huo utawanufaisha wakazi 2,514 ikiwemo wanafunzi  557 wa shule ya Msingi Iwafi na  259  wa shule ya sekondari Idamba.

Akizungumza katika mkutano wa Hadhara na wananchi katika kijiji cha Iwafi kata ya Idamba wilayani Njombe Mhandisi Kamwelwe aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maji na kuwataka wananchi kuhakikisha wanaitunza miradi hiyo.

“Nimeridhishwa na matumizi yenu ya fedha pamoja na utekelezaji wa miradi ya maji, nawapongeza sana endapo mtaendelea kutumia fedha hivi mwaka ujao tutawaongezeeni” alisema Mhandisi Kamwelwe.

“ Kutokana na miradi ya kutumia mashine za diesel  kuwa na gharama kubwa nawashauri wakati mwingine mtumie umeme wa nguvu za jua japo najua huku kuna baadhi ya maeneo yana  changamoto ya hali ya hewa” aliongeza Mhandisi Kamwelwe.

Mradi maji katika kijiji cha Iwafi  unatekelezwa kwa pamoja  baina ya shirika la Peoples’ Development Forum (PDF) kwa ushirikiano wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe na wananchi wa  kijiji cha Iwafi kupitia  programu ya mradi wa Maji, Afya na Usafi wa mazingira unaofadhiliwa na shirika la UNICEF.

Kazi ambazo zimekamilika hadi sasa katika mradi huu ambao utaendeshwa kwa  mashine ya mafuta ya diesel kusukuma maji ni pamoja na ujenzi wa tanki lakukusanyia maji kwenye chanzo, ufungaji wa mashine ya kusukumia maji, uchimbaji wa mitaro na ulazaji wa mabomba kwenye eneo lenye urefu wa mita 11934.

Upande wa ujenzi wa tanki la kutawanya maji  kwenye vitongoji sita lenye ujazo wa lita elfu 50 upo katika hatua ya ukamilishaji na linatarajiwa kukamilika hivi karibuni na kuanza kutoa huduma kwenye kijiji cha Iwafi.

Katika kufanikisha mradi huu jamii imechangia nguvu kazi ikiwemo uchimbaji wa mitaro, kulaza mabomba na kuyafukia ,  usombaji wa mawe , ufyatuaji wa tofari ambavyo vyote kwa pamoja vina thamani zaidi ya milioni 25. Michango mingine inatoka kwa UNICEF na PDF ambao  wanachangia  zaidi ya milioni 155 na  Halmashauri ya wilaya ya Njombe wanachangia zaidi ya milioni 50.

Akiwa katika ziara ya siku moja katika halmashauri ya wilaya ya Njombe Mhandishi Kamwelwe alikagua vituo vya maji vilivyofungwa mita katika eneo la Lupembe barazani ikiwa ni ufuatiliaji wa agizo la Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa ambalo alilitoa alipokuwepo katika ziara wilayani Njombe. Aidha,   alipata nafasi ya kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo ya Iwafi na Lupembe na kutolea ufafanuzi masuala mbalimbali yaliyoulizwa na wananchi.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa