• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Milioni 61 zatolewa kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Njombe

Tarehe iliyowekwa: November 29th, 2017

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 61 kwa vikundi vya wanawake na vijana ikiwa na lengo la kuongeza kipato na kuwainua kiuchumi.

Mikopo hiyo ambayo imetolewa kwa  awamu ya kwanza  ya  mwaka wa fedha 2017/2018 kupitia mfuko wa maendeleo ya vijana (YDF) na ule wa wanawake (WDF) umevinufaisha vikundi 52 vya vijana na wanawake wilayani Hapa.

Kupitia  mikopo hiyo vikundi   35 vya wanawake  vimepewa mkopo wenye thamani ya shilingi milioni 40 huku upande wa vijana vikundi 17 vikipewa  milioni 21.

Mikopo iliyotolewa imetokana  na fedha ya bakaa  ya mwaka 2016/2017 kiasi cha shilingi milioni 28, marejesho ya mikopo iliyotolewa awali kiasi cha milioni 25 huku mchango wa Halmashauri unaotokana na mapato ya ndani kwa   kipindi cha mwezi Julai  hadi Septemba 2017/2018  ukiwa ni milioni 13.

Mikopo hii imepitishiwa katika  vyama vya akiba na mikopo (SACCOS) vilivyo jirani na walengwa kwa lengo la kurahisisha zoezi la  ukopeshaji na urejeshaji ikiwa ni pamoja na kuwapunguzia wakopaji gharama za ufuatiliaji wa mikopo Makao makuu ya wilaya Njombe Mjini.


Upitishaji huu wa mikopo kwenye SACCOS una lengo la  kuipunguzia Halmashauri gharama za ufuatiliaji wa madeni hayo pamoja na kuwawezesha Vijana na Wanawake kujenga tabia ya kuweka akiba na kukopa katika SACCOS zilizo jirani nao badala ya kutegemea Mfuko wa Maendeleo ya Vijana na Wanawake tu.


Akizungumza na vikundi vya wanawake na vijana wakati wa kukabidhiwa hundi za mikopo hiyo Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Bi Ruth Msafiri ambaye alikua mgeni rasmi alivitaka vikundi vilivyopewa mikopo kuitumia vizuri ili kuweza kujikwambua kiuchumi.


 “Naomba mkatumie mikopo hii kwa malengo mliyokusudia na miradi iliyopitishwa na wataalamu kwa kuwa  serikali inatoa mikopo hii kwa riba ndogo kwa lengo la kuwainua kiuchumi, mkumbuke kuwa hii sio zawadi lazima irudishwe ili na wenzenu waweze kupewa” alisema  Msafiri.


Aliwataka maafisa ugani wilayani hapa kuvisaidia vikundi vya kilimo na ufugaji kuendesha shughuli zao kisasa pamoja na kuacha kufanya biashara kwa mazoea ili malengo ya mikopo hiyo yaweze kutiamia.


Awali akisoma taarifa ya mfuko wa wanawake na vijana  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Bi  Monica Kwiluhya alisema mikopo inayotolewa imeweza kuongeza mitaji ya shughuli na miradi ya vikundi ikiwemo  kilimo cha mazao mbalimbali, Ufugaji wa mifugo , Ushonaji nguo, migahawa na vitalu vya miche ya miti mbalimbali.


“Kupitia Mifuko hii vijana na wanawake wameweza kuunganishwa na taasisi mbalimbali za kifedha kama vile SACCOS, VICOBA na benki ya Wananchi Njombe (NJOCOBA)” alisema Kwiluhya


Akizungumzia changamoto zinazoikabili Halmashauri katika utoaji wa mikopo hiyo alisema kuwa  baadhi ya wanakikundi hutumia mkopo kinyume na miradi waliyoiombea,  hivyo miradi hiyo hushindwa kuwa na tija na hatimaye hushindwa kurejesha mikopo kwa wakati.


Kuhusu ufumbuzi wa changamoto hiyo Kwiluhya alisema kuwa kabla ya vikundi kupewa mikopo Halmashauri inavijengea uwezo  kwa kuvipatia elimu ya ujasiriamali pamoja na umuhimu wa kujiunga na SACCOS kwa lengo la kupata fursa nyingine ya kuweka akiba na kukopa ili waweze kuzalisha zaidi.


Mikopo inayotolewa ina lengo la kuwaongezea mitaji Vijana na Wanawake na Riba yake ni 10%. Tangu mwaka 2006 hadi sasa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imetoa mikopo yenye zaidi ya shilingi milioni  561 kwa vikundi vya vijana na wanawake ambapo zaidi ya milioni  160  zimetolewa kwa vikundi 168 vya vijana na zaidi ya milioni   401 kwa vikundi 507 Vya wanawake.







Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa