• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Madiwani waomba ufafanuzi kuhusu kuchelewa kwa fedha za Vijiji Njombe

Tarehe iliyowekwa: November 2nd, 2017

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya  Njombe limeridhia ufafanuzi uliotolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Monica Kwiluhya baada ya kumwagiza kutoa ufafanuzi kuhusu utumwaji wa fedha za asilimia 12 kwenye maeneo ya vijiji ambao ulikuwa haujafanyika kwa wakati .

Hali hii ilitokea wakati wa kufungua mkutano wa baraza la madiwani ambapo  hufanyika kwa siku mbili huku siku ya kwanza ikiwa ni maalumu kwa kupokea taarifa ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali kwenye maeneo ya Kata ambazo  uwasilishwa na diwani wa Kata husika.

Kufuatia kuchelewa kutumwa kwa asilimia hizo kwenye Kata  madiwani walitaka ufafanuzi kutoka kwa mkurugenzi wa sababu zilizopeleka jambo hilo ambapo mkurugenzi pamoja na wataalamu walitoa ufafanuzi kuwa  changamoto kubwa ni suala la mtandao

Hali hiyo ilipelekea baraza hilo kujigeuza kama kamati ambapo walimwagiza Mkurugenzi kuandaa taarifa ya kiasi kinachodaiwa kwenye kila  Kata pamoja na sababau zilizopeleka kuchelewa kutumwa kwa asilimia hizo.

Akitoa ufafanuzi siku ya pili ya  mkutano wa   baraza la madiwani , Kwiluhya alisema kuwa sababu iliyopelekea kuchelewa kulipwa kwa asilimia hizo ni matatizo ya mfumo wa kupokelea mapato kuanzia mwezi Julai hadi Octoba hali iliyopelekea Halmashauri kushindwa kurudisha asilimia hizo kwa wakati.

“Mheshimiwa mwenyekiti kutokana na tatizo la mfumo Halmashauri iliwasiliana na ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Njombe pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa tukiomba kutatuliwa kwa changamoto hii ili Halmashauri kutekeleza majukumu yake” alisema Bi Kwiluhya.

“Tayari katibu mkuu  ameleta wataalam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kushughulikia  changamoto hizi wakisaidiana na wataalam wetu na kwa sasa tatizo limeanza kupungua na malipo yameandaliwa”  Aliongeza Kwiluhya.

Alifafanua kuwa kilichochelewesha kulipwa kwa asilimia  hizo ni usuluhishi wa fedha kati ya mashine za kukusanyia mapato na taarifa ya mapato yanayosomeka katika mfumo  kwenye ofisi kuu ya Halmashauri na kutaja kiasi kinachodaiwa na vijiji kuwa ni milioni 32 ikiwa ni fedha ya  Mwezi Machi hadi June 2017.

Katika kukabiliana na changamoto hiyo alisema kuwa Halmashauri kwa sasa imefanya mawasiliano na wamiliki wote wa simu za kukusanyia  mapato kutoa ripoti ya kila siku ili kurahisisha  usuluhisho wa miamala kati ya Halmashauri na wakusanyaji wakati wa uwasilishaji wa mapato jambo litakalosaidia upelekeaji wa asilimia hizo kwa wakati.

Mwaka wa fedha 2017/2018 katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe  asilimia 12 za mwezi Julai na Agosti zimeshalipwa huku ile ya mwezi septemba yenye kiasi cha 10,953,936 hundi imeandaliwa kwa malipo.




Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa