• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Madiwani Geita wazipongeza SACCOS Njombe

Tarehe iliyowekwa: June 30th, 2017

Madiwani wa  Halmashauri ya wilaya ya Geita  na wataalamu wa Halmashauri hiyo wamezipongeza  SACCOS  Zilizoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kutokana na ubunifu na utendaji mzuri wa kazi kwa kushirikiana na Halmashauri katika kuwakwamua wanawake na vijana wilayani Njombe.

Pongezi hizo zimetolewa wakati wa ziara  waliyoifanya katika Halmashauri ya wilaya ya Njombe ikiwa na lengo la kujifunza namna mifuko ya wanawake na vijana inavyofanya kazi katika Halmashauri hii.

Akizungumza katika ziara hiyo mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Geita ,Bw. Elisha Lupuga alisema kuwa wamejifunza kitu kikubwa ambacho wanakwenda kukifanyia kazi katika Halmashauri yao.

"Kiukweli safari yetu imekuwa na manufaa makubwa kwani tumejifunza mambo mengi mazuri, tumepata elimu  na tukitoka hapa tunakwenda kufanya mambo makubwa huko kwetu na tutawaalika mje kuona baada ya muda mfupi, sisi kule tuna majimbo mawili hivyo tunaweza kuanza na SACCOS moja kwa kila jimbo " alisema Bw. Lupuga.

"Hongereni sana SACCOS zenu ziko kama benki tu kwa muonekano pamoja na huduma zinazotolewa, hakika somo limeingia" aliongeza Bw. Lupuga.

Awali akisoma taarifa kuhusu namna mfuko wa wanawake na vijana unavyofanya kazi katika Halmashauri ya Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Bi Monica P.Z Kwiluhya, alieleza kuwa toka mwaka 2006 hadi 2017 Halmashauri imefanikiwa kutoa mikopo yenye thamani zaidi ya Milioni 400 kwa vikundi zaidi ya 500 vya wanawake na vijana.

Aliongeza kuwa mikopo hii hutolewa kupitia SACCOS zilizo jirani na walengwa kwa lengo la kurahishisha zoezi zima la ukopeshaji na urejeshaji ikiwa ni pamoja na kuwapunguzia gharama za ufuatiliaji wilayani wakopaji  na kuipunguzia gharama Halmashauri za ufuatiliaji wa madeni hayo pamoja na kuwajengea vijana na wanawake tabia ya kuweka akiba na kukopa katika SACCOS zilizo jirani nao badala ya kutegemea mfuko wa maendeleo ya vijana tu.

Alieleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri imekopesha jumla ya shilingi Milioni 114,500,000 kwa vikundi 88 huku vikundi vya wanawake vikiwa 61 na kupata Milioni 68 na vijana vikundi 27 vikipata 46 milioni huku mchango wa Halmashauri ukiwa zaidi ya milioni 80 ambazo ni sawa na zaidi ya asilimia 82 ya fedha zilizokisiwa kuchangwa kupitia mapato ya ndani.

Kuhusu mafanikio ambayo yametokana na na mikopo inayotolewa kwa vikundi vya vijana na wanawake watanowatano kwa lengo la kuzikwamua familia  Bi Kwiluhya alisema kuwa wanavikundi wengi wameongeza mitaji yao na kupanua shughuli wanazofanya ikiwemo kilimo, ufugaji wa mifugo mbalimbali , ushonaji nguo, migahawa ,kulipa ada pamoja na kuboresha makazi.

" Halmashauri imeweza kuviunganisha vikundi vya vijana na wanawake na taasisi mbalimbali za kifedha kama vile SACCOS, VIKOBA, Benki ya wananchi Njombe  pamoja na taasisi nyingine" aliongeza Bi Kwiluhya.

Katika  ziara hiyo madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita pamoja na watalumu wa Wilaya hiyo  walitembelea SACCOS ya Nyombo iliyopo katika kijiji cha Nyombo kata ya Ikuna ,SACCOS ya Ibumila iliyopoa Kijiji cha Ibumila Kata ya Kichiwa Pamoja na kikundi cha Ushonaji Nguo Nyombo kilichopo kijiji cha Nyombo.

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina jumla ya SACCOS 12 na mikopo ya wanawake na vijana inalengo la kuwainua vijana na wanawake kiuchumi pamoja na kuwaongezea mitaji huku liba yake ikiwa ni asilimia 10 tu

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa