• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

Tarehe iliyowekwa: January 24th, 2025



Changamoto ya kutowalipa wakulima na wafanyakazi wa sekta ya chai mkoani Njombe imetajwa kusababisha baadhi ya wakulima kutelekeza mashamba ya chai na kujikita kupanda mazao mengine.

Baadhi ya viwanda hivi sasa vinaonekana kutofanya kazi na vingine kushindwa kuwalipa wakulima na wafanyakazi wao hatua iliyochagiza wakulima kukiona Kilimo Cha chai mwiba mkali.

Migomo ya wafanyakazi kwenye viwanda vya chai mkoani Njombe imekuwa ya mara kwa mara ikisababishwa na kucheleweshewa Mishahara yao na kusababisha serikali kuingia lawamani.
Katika Kikao Cha Ushauri wilaya ya Njombe DCC kilichoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa , Baadhi ya wadau wa chai na wakulima wamevitupia lawama viwanda na wawekezaji wa chai huku wakitaka hatua za maksudi Kuchukuliwa ili kunusuru adha kwa wakulima na wafanyakazi.

Baadhi yao ni Mzee Lukule Mponji,Yotham Mhiche,Ally Mhagama na Mchungaji Nelson Godiwe wameishauri na kuitaka Serikali kuendelea kulifanyia kazi changamoto zinazowakuta wakulima na kupelekea kupotea kwa thamani ya zao la chai.

Aidha Mbunge wa Jimbo la Lupembe  Edwin Swalle amemuunga mkono Mhe. Kissa kuundwa kwa Tume itakayochunguza mkwamo wa viwanda vya Chai Njombe ili kupata suluhu ya Kudumu ili kunusuru sekta hiyo.

Theofhord Ndunguru mkurugenzi mkuu Wakala wa Maendeleo ya wakulima wadogo wa Chai nchini anasema Kuporomoka kwa soko la zao Hilo  duniani kutokana na kushuka kwa unywaji wa chai kuliko uzalishaji Na hivyo kumesababisha  adha kubwa kiuchumi jambo linalosabisha wakulima na wafanyakazi Wengi kulalamika.

Ndunguru  amesema viwanda vingi vya chai duniani vikiwemo vya Kenya Uganda na Tanzania vimefungwa kutokana na hasara kubwa ya uendeshaji.

Naye Jaherson Moturi ni mkurugenzi wa viwanda vya Chai vya Kampuni ya DL Group ambaye amekiri kuchelewesha malipo ya wafanyakazi na kwa kiwanda Cha kibena wanadaiwa Mishahara ya Mwezi Mmoja Ambayo Wanatarajia kuilipa hivi karibuni na Ikanga Lupembe miezi miwili.

Kutokana na changamoto hizo mkuu wa wilaya ya Njombe Kissa Kasongwa amelazimika kuunda Kamati maalumu ya uchunguzi itakayofanya kazi ya kufuatilia changamoto za viwanda vya chai ili ije na majibu sahihi yatakayowasaidia wakulima na wafanyakazi kupata Fedha zao.








Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa