• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Ijue Kamapeni ya Afya na Usafi wa Mazingira Njombe

Tarehe iliyowekwa: August 20th, 2018

Mbali na kuwa na sifa katika utunzaji wa mazingira ambao unakwenda sambamba na upandaji wa miti na kuifanya wilaya hii kuwa ya kijani, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe inasifika kwa kuwa kinara katika utekelezaji wa kampeni ya afya na usafi wa mazingira nchin Tanzania.

Haikuwa lahisi kwa Halmashauri hii kuweza kufikia mafaniko haya bali imetokana na umoja na mshikamano uliopo baina ya viongozi kuanzia wale wa chama na serikali. Ilikuwaje hadi Halmashauri hii ikafanikiwa kuwa kinara katika utekelezaji.

Kampeni ya Kitaifa ya afya na usafi wa mazingira nchini Tanzania ilizinduliwa na Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete mwaka , 2012 mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro.

Kampeni hii ililenga kuinua kiwango cha upatikanaji wa huduma bora za usafi wa mazingira kwa kuinua uwiano wa kaya zenye vyoo bora kwa zaidi ya asilimia 50% hadi hadi kufikia mwaka 2015.

Sambamba na kuinua kiwango cha upatikananji wa huduma bora za usadi wa mazingira pia ililenga kupunguza kuenea kwa magonjwa yasababishwayo na mazingira machafu (Sanitation related diseases).

Awamu ya kwanza imetekelezwa katika ngazi ya kaya na katika shule za msingi na ililenga kuhakikisha kuwa kila kaya katika eneo la kampeni inakuwa na vyoo bora pamoja na miundombinu ya kunawa mikono baada ya kutoka chooni.

Ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kampeni hii inatekelezwa katika Kata zote 12, vijiji 45 na vitongoji 227. Aidha, kampeni hii inatekelezwa katika shule 53 za msingi za serikali zilizoko katika Halmashauri.

Katika ngazi ya jamii na kaya mambo mbalimbali yamefanyika ili kuweza kufanikisha kampeni  ikiwemo kutoa mafunzo kwa viongozi wa Halmashauri (Wajumbe wa baraza la ushauri la wilaya (DCC), Baraza la madiwani, wakuu wa Idara na vitengo pamoja na wadau mbalimbali waliopo katika Halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Aidha,  mafunzo kwa timu ya usimamizi wa kampeni ngazi ya Wilaya ikijumuisha wataalam kutoka idara ya Afya, maji, elimu msingi na Maendeleo ya Jamii yametolewa ili kuweza kufanikisha malengo ya kampeni na kuwa na jamii yenye afya bora kutokana na kuepukana na magonjwa yatokanayo na uchafu.

Ili kuweza kufanikisha kampeni ,Halmashauri ilitoa mafunzo ya utekelezaji wa kampeni kwa viongozi wa kata,vijiji na vitongoji vyote pamoja na wahudumu wa afya katika vijiji vyote vya kampeni pamoja na kukusanya takwimu za usafi wa mazingira na kuziingiza katika rejista maalum za kitongoji.

Sambamba na hilo  mikutano ya uhamasishaji (uchefuaji) ilifanyika katika vitongoji vyote 227 vilivyopo katika Halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Kutokana na kampeni hii kuhusisha Nyanja mbalimbali mafunzo yalitolewa kwa mafundi ujenzi juu ya ujenzi wa vyoo bora ili kuhakikisha ujenzi wa vyoo unazingatia kanuni zote za afya na usafi wa mazingira.

Baada ya kamapeni na  ufuatiliaji wa mara kwa mara unafanyika  ili kuona maendeleo ya utekelezaji wa kampeni pamoja na kufanya vikao mbalimbali vya tathmini ya utekelezaji na kubadilishana uzoefu kati ya viongozi wa vitongoji, vijiji, kata, Wilaya na wadau mbalimbali wa usafi wa mazingira katika Halmashauri jambo lililochangia mafanikio makubwa kwenye usafi.

Hali hii imepelekea Halmashauri ya wilaya ya Njombe kuwa kinara kwenye utekelezaji wa kampeni ya afya na usafi wa mazingira nchini Tanzania na kuwa miongoni mwa Halmashauri za mafano kwa kuwa na vyoo bora kuanzia ngazi za Kaya, vijiji na Kata.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa