• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Halmashauri ya wilaya ya Njombe yatoa mshindi wa Pili Kanda Maonesho ya Nane nane

Tarehe iliyowekwa: August 8th, 2019

Halmashauri ya wilaya ya Wilaya ya Njombe imefanikiwa kutoa  mshindi wa kwanza Mkoa wa Njombe  na mshindi wa pili Kikanda katika kundi la wafugaji wa N'gombe wa maziwa na samaki kwenye maonyesho ya nane nane mwaka 2019.

Katika maonyesho hayo ambapo mgeni rasmi alikuwa waziri mkuu mstaafu Mizengo Kayanza Peter Pinda  ambapo  Bi Raheli Mhema kutoka katika Kijiji cha Ikando kilichopo kwenye Kata ya Kichiwa Halmashauri ya wilaya ya Njombe amefanikiwa kushinda nafasi ya kwanza mkoa wa Njombe na nafasi ya pili Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.

Akizungumza baada ya kushinda Bi Mhema alieleza  kuwa alianza shughuli ya ufugaji mwaka 2013 baada ya kupewa Ng’ombe wa maziwa na Halmashauri ya wilaya ya Njombe kupitia mpango wa maendeleo ya kilimo (DADPs)

Alisema kuwa  mwaka 2015 alikwenda Mbeya kwenye maonyesho kwa ajili ya kujifunza zaidi masuala ya ufugaji bora na wakisasa ambapo aliboresha banda pamoja na malisho ya Ng’ombe.

“ Baada ya kupewa elimu kutoka kwa wataalamu wa Halmashauri ya Njombe  nilianza ufugaji ambapo kwa sasa nina Ng’ombe wanne wadogo wako wawili na wakubwa wawili” alieleza Bi Mhema

Aliongeza kuwa sasa ana ng’ombe wake ambaye anauwezo wa kuzalisha maziwa lita 30 kwa siku ambapo asubuhi anatoa lita 17 na jioni 13  na kumpatia zaidi ya 780 kwa mwezi na  milioni 9 kwa mwaka  baada ya kuondoa gharama za uendeshaji.

“  Upande wa ufugaji ukitoa gharama za uzalishaji ninapata zaidi ya milioni tisa na kilimo Napata zaidi ya milioni 6 nikitoa gharama za uendeshaji hivyo nakusanya zaidi ya milioni 15 kupitia kilimo na ufugaji” alibainisha Bi Mhema.

Kuhusu soko la maziwa Bi Mwenda alisema kuwa anauza maziwa yake katika kiwanda cha Njombe Milk Factory kilichopo Njombe mjini na kuwa na uhakika wa soko.

Akizungumzia kuhusu mafanikio aliyoyapata kupitia ufugaji Bi Mhema alisema kuwa ameweza kujenga nyumba nzuri, kununua usafiri pamoja na kusomesha watoto.

“Mtoto wangu wangu wa Kwanza amemaliza chuo cha uuguzi na mwingine yupo kidato cha tano, fedha zingine nanunulia mashamba na kuwekeza kwenye kilimo” alisema Bi Mhema

Ametoa wito kwa jamii kujikita katika  kilimo na ufugaji wenye tija na  kisasa  ili kuinua kipato cha taifa na familia kwa ujumla.

Maonyesho ya nane nane yamefanyika Mkoani Mbeya ambapo yamehusisha Mikoa ya Nyanda za Juu kusini ikiwemo Njombe, Ruvuma, Iringa, Mbeya, Songwe Rukwa  huku yakiwa na kauli mbiu inayosema Kilimo, mifugo na Uvuvi kwa ukuaji wa uchumi wa nchi".




Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa