• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe yapongezwa kwa kupata hati safi hesabu za 2015/2016

Tarehe iliyowekwa: August 16th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka ameipongeza Halmashauri ya Wilaya Njombe kwa kupata hati safi katika hesabu za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2015/2016.

Pongezi hizo alizitoa katika baraza maalumu la madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Njombe la kujadili taarifa na mpango kazi wa hoja za Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali lililofanyika wilayani Njombe.

Akizungumza katika baraza hilo Ole Sendeka alisema kuwa anaipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa kupata hati safi kwa mahesabu ya jumla na hati zinazoridhisha kwa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa kipindi cha mwaka 2016/2017.

“Nitoe pongezi za dhati kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya, Baraza la M

adiwani, Mkurugenzi Mtendaji pamoja na wataalamu wake kwa kazi nzuri mnazofanya. Katika mkoa wangu kuna Halmashauri sita, tano zimepokea hati safi na moja hati yenye mashaka kwenye hesabu za serikali katika mwaka wa fedha 2015/2016 na nyinyi ni miongoni mwa halmashauri zilizopata hati safi". Alisema Ole Sendeka.

“Miradi yenu inakidhi viwango kwani niliitembelea na kuiona katika ziara yangu nilioifanya katika Halmashauri yenu, naomba kila mtu ajue namna ya kuitumia nafasi yake kama mtumishi wa Umma, kuimarisha mifumo ya ndani ya mapato na usimamizi ili kuzidi kuboresha na kuendeleza miradi”  aliongeza Ole Sendeke

Alizitaka halmashauri kuendeleza uwazi na uwajibikaji  kwa kufuata matumizi sahihi ya fedha kwa kuzingatia  taratibu zilizowekwa na serikali.

“Uwazi na uwajibikaji ni mkataba wetu na wananchi kupitia Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, Sehemu nyingine nimewasimamisha kazi watumishi,  bora kuwa na watumishi wachache wachapakazi kuliko watumishi wengi wasiofanya kazi, lakini kwa upande wenu mnafanya kazi nzuri na ninafurahi na kuwapongeza sana” alisema Ole Sendeka

Awali akifungua baraza  maalumu la Madiwani Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Bw Valentino Aidan Hongoli alisema kuwa Halmashauri imepata hati safi kwa hesabu za jumla pamoja na kupata hati zinazoridhisha katika miradi ya maendeleo ikiwemo barabara, maji, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ,kilimo na mifugo pamoja na mfuko wa pamoja wa afya (Health basket fund).

Aliongeza kuwa Halmashauri imejipanga kuhakikisha kuwa inafanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa na Mkaguzi Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuyawekea mipango na kuitekeleza kwa mafanikio ambayo yataleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo.

Mwaka wa 2015/2016 katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe zilitolewa hoja 51 na hoja 22 za miaka ya nyuma. Kati ya hoja 38 zimehakikiwa na mkaguzi na kufungwa sawa na asilimia 74.51 ,hoja 13 zipo katika hatua ya utekelezaji sawa 25.49%. Hoja 12 kati ya zile 22 za miaka ya nyuma zimeakikiwa na kufungwa na hoja 10 zinazosalia ni zile ambazo zipo katika hatua za utekelezaji.

Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imejipanga kuhakikisha enaendelea kupata hati safi na kufanya vizuri katika nyanja mbalimbali ili kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa