• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Kufanya mikutano ya kusikiliza kero za Wananchi Kata Zote

Tarehe iliyowekwa: November 13th, 2017

Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya  ya  Njombe umefanya mkutano wa hadhara katika Kata ya Lupembe ikiwa ni utaratibu ulioanzishwa kwa lengo la kupokea na kusikiliza Kero na changamoto mbalimbali zilizopo katika Kata zake.

Katika mkutano huo ambao ulimjumuisha mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe , Valentino Hongoli, Mkurugenzi mtendaji Monica Kwiluhya pamoja na wataalamu kutoka katika ngazi ya Halmashauri, Kata na Kijiji cha Lupembe ambapo wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali katika maswala mtambuka pamoja na kutoa changamoto zinazowakabili katika kata yao.

Akijibu changamoto ya wodi la kina mama katika kituo cha afya Lupembe ambalo bado halijakamilika, Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe, Monica Kwiluhya aliahidi hadi kufikia mwezi Desemba mwaka huu wodi hiyo itakuwa imekamilika na kuanza kutumika.

“Halmashauri inafanya jitihada kubwa kuhakikisha wodi ya kinamama inakamilika  nawahakikishia wodi hii itakamilika mwaka huu na nyinyi wenyewe ni mashahidi kwa kazi kubwa tuliyoifanya katika kituo chenu, Naomba tushirikiane kujenga shimo la maji machafu” alisema Kwiluhya

“Halmashauri inafanya mpango wa kupata jenereta kwa ajili ya chumba cha upasuaji katika kituo cha afya Lupembe ambapo upasuaji umeanza kufanyika, Tumepoteza wakinamama na watoto wengi sasa huduma ya upasuaji imeanza tunaomba mkawe mabalozi wazuri na kukitumia vizuri kituo chenu” aliongeza Kwiluhya.

Akizungumzia changamoto ya maji na miundombinu yake katika Kata ya Lupembe alisema kuwa tayari jumuiya ya watumia maji imeshaundwa na inafanya kazi. Alisema kuwa wataalamu wa Halmashauri wamepita kufanya upembezi kwa ajili ya kuweka katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 ili   kuboresha miundombinu ya maji na  kuweza kukidhi mahitaji katika kata ya Lupembe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Valentino Hongoli aliwataka wananchi wa Lupembe kushiriki katika maendeleo na kutoitegemea serikali pekee katika kutekeleza mira kwenye maeneo yao.

“Tunaomba mtoe ushirikiano na wataalumu waliopo katika Kata hii kuweza kutatua matatizo yaliyopo  ndani ya uwezo wenu badala ya kusubili serikali, kufanya hivyo tutakuwa tunachelewesha maendeleo katika Kata yetu.” alisema Hongoli.

Kupitia mkutano huo  wananchi  wa Kata ya Lupembe wameishukuru Halmashuri ya Wilaya ya Njombe kwa kuanzisha huduma ya upasuaji kwa akina mama wajawazito katika kituo cha afya Lupembe  ambapo hadi kufikia ijumaa ya wiki iliyopita akina mama tisa walikuwa  wamekwisha fanyiwa upasuaji  na wanaendelea  vizuri.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa