• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Bilioni Moja Kujenga Mradi wa Maji Kijiji cha Kidegembye Njombe

Tarehe iliyowekwa: July 18th, 2018

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe inatekeleza ujenzi wa mradi mkubwa wa maji katika kijiji cha Kidegembye wilayani Njombe ambapo hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya bilioni moja.

Ujenzi wa Mradi huo unagharamiwa  na mfuko wa maji uliochini ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji , unajengwa na  mkandalasi M/S STC Construction Limited utakamilika  Novemba 2018 ambapo  unatarajia kuhudumia watu zaidi ya  6,362 kwa kipindi cha miaka 20 ijayo .

Katika utekelezaji wa mradi huu wananchi wa kijiji cha  Kidegembye wanachangia asilimia 2.5 ya gharama za mradi ambazo ni sawa na zaidi ya milioni 33 fedha ambazo zitatumika kuendeshea mradi baada ya kukabidhiwa.

Hadi sasa  ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa lita laki moja na urefu wa mita sita uko katika hatua ya upigaji plasta, huku ujenzi wa mtego wa maji na nyumba ya pampu ukiwa katika hatua ya ukamilishaji.

Aidha, vifaa vyote kwa ajili ya mradi viko kwenye eneo la mradi  ikiwemo mabomba yenye urefu wa mita 17 elfu huku  uchimbaji wa mtaro na ulazaji wa bomba kuu ukikamilika na kazi inayoendelea ni upelekaji wa mabomba mitaani kwa wananchi.

Mbali na kunufaika kwa kupata huduma ya maji safi na salama, wananchi wa Kidegembye watapata manufaa ya fedha za kuanzia gharama za uendeshaji wa mradi huu baada ya kuingia mkataba na mkandalasi kwa kuchimba na kufukia mtaro ambapo fedha zitatazopatikana na kazi hiyo  zitaingia kwenye mfuko wa Jumuiya ya watumia maji kama mchango wa wananchi kwa ajili ya usimamizi na uendeshaji wa mradi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa kijiji cha Kidegembye wameishukuru Serikali kwa kuwaletea mradi mkubwa wa maji ambao utasaidia kusukuma maendeleo kutokana na kuwa na uhakika wa maji safi na salama.

Halmashauri ya wilaya ya Njombe hadi sasa inajumla ya miradi 72 ya maji inayotumia teknolojia mbalimbali katika kutoa huduma ya maji safi na salama. Miradi inayotumia teknolojia ya maji mtiririko ipo 11, inayotumia mashine ya dizel ipo mitano,  nishati ya umeme iko mitano.

Sambamba na hiyo miradi saba inatumia hydram inayosukumwa na nguvu ya maji, miradi mitatu inatumia nguvu ya maji kwa kutumia magurudumu ijulikanayo kama water wheel , huku miradi ya visima vifupi ipo  33 na  virefu iko 8.

Kutokana na miradi hii watu 51,448 kati ya watu 85,747 sawa na asilimia 60 ya wananchi waliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe wanapata huduma ya maji.

Aidha, asilimia ya huduma ya maji imepanda kutoka 54.9 ya mwaka 2016/2017 hadi kufikia asilimia 60 mwaka 2018 kutokana na kukamilika kwa mradi wa maji katika  kijiji cha Iwafi pamoja na uchimbaji wa kisima kirefu katika shule ya Msingi Kidegembye.



Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa