• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Bilioni 27 kutekeleza shughuli za maendeleo Halmashauri ya Wilaya Njombe

Tarehe iliyowekwa: February 25th, 2019

Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Njombe limepitisha rasimu ya mpango na bajeti yenye kiasi cha Bilioni 27.4  kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali katika mwaka wa fedha 2019/2020.

Katika rasimu hiyo ya bajeti kiasi cha bilioni 20.7 ni ruzuku ya mishahara, ruzuku ya matumizi mengineyo ikiwa ni bilioni 1.084 , ruzuku ya miradi ya maendeleo ikiwa ni bilioni 3.1  huku mapato ya ndani ikiwa ni bilioni 1. 5 ambayo ni mapato halisi, milioni 465 ni mapato maalum na mchango wa jamii ni milioni 523.

Aidha, Halmashauri ya wilaya ya Njombe inatarajia kutumia kiasi cha Bilioni 3.7 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri.

Katika fedha hizo zaidi ya milioni 609 ni mchango wa Halmashauri wa asilimia 40 ya mapato halisi ya ndani, Bilioni 2.4 ni fedha za ruzuku kutoka Serikali kuu na kiasi cha milioni 699 ni fedha za wafadhili.

Akiwasilisha bajeti katika baraza maalum la madiwani , Afisa mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Anganile Daniel alisema kuwa bajeti ya mwaka 2019/2020 imeongezeka kwa asilimia 18 ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2018/2019 ambayo ilikuwa ni Bilioni 22.5

“Mheshimiwa mwenyekiti ongezeko la bajeti  limetokana na  kuongezeka kwa makisio ya vyanzo vya mapato ikiwa ni pamoja na bajeti ya mishahara ambayo imeongezeka kutoka  bilioni 15.7 kwa mwaka wa fedha 2018/2019 hadi kufikia bilioni 20.7  kwa mwaka wa fedha 2019/2020 sawa na ongezeko la asilimia 24” alisema Daniel

“Upande wa   makisio ya  mapato halisi ya ndani  yameongezeka kutoka bilioni 1. 4 kwa mwaka 2018/2019 hadi kufikia bilioni 1.5 kwa mwaka wa fedha 2019/2020” alifafanua Daniel

Daniel alibainisha kuwa kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri ya wilaya ya Njombe imewasilisha maandiko ya maombi maalum ya miradi ya kutoa huduma yenye thamani zaidi ya bilioni 15 ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya serikali ya kuandaa maandiko ya miradi ya kutoa huduma kwa jamii.

Miradi inayotarajiwa kutekelezwa ni pamoja na Ukamilishaji wa ujenzi wa zahanati 6 za Upami, Itunduma, Welela, Havanga, Igombola, Lima, kituo cha Afya Ikuna na jengo la mama na  mtoto (RCH) katika zahanati ya Mfriga.

Miradi mingine ni ujenzi wa vyoo bora katika vituo 21 vya kutolea huduma za afya, ujenzi wa Miradi ya maji katika vijiji vya Kanikelele, Ikang’asi na Ikuna, ujenzi wa vyumba 52 vya madarasa ya shule za msingi pamoja na ujenzi wa nyumba 10 za walimu wa shule 10 za msingi (two in one)

Sambamba na hilo upo Ujenzi wa mabweni 2 katika shule ya msingi Matembwe, Ujenzi wa matundu 157 ya vyoo katika shule 6 za Sekondari, Ujenzi wa nyumba 249 za walimu wa shule 11 za Sekondari (two in one)

Kuhusu miradi ya kimkakati, Daniel  alieleza kuwa kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe imewasilisha TAMISEMI andiko la mradi wa ujenzi wa jengo la kibiashara ambalo linatarajiwa kujengwa katika eneo lililopo pembezoni mwa zilipo ofisi za makao makuu ya Halmashauri.

Halmashauri ya wilaya ya Njombe inakata 12 zenye vijiji 45.











Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa