• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
NJOMBE DISTRICT COUNCIL
NJOMBE DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Maliasili na Ardhi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
    • Kata
    • Vijiji
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Misitu na Upandaji Miti
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Biashara
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ardhi na Maliasili
    • Uwezeshaji kwa Wananchi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi
    • Ratiba ya Vikao
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyopendekezwa.
    • Miradi Inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti Mbalimbali
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
    • Hotuba
    • Habari
    • Tukio
    • Gazeti/Jarida

Bilioni 26 kutekeleza Shughuli mbalimbali Njombe mwaka 2020

Tarehe iliyowekwa: January 24th, 2020

Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Njombe limepitisha mpango na bajeti wenye kiasi cha zaidi ya bilioni 26 kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali katika mwaka wa fedha 2020/2021.

Katika bajeti hiyo kiasi cha bilioni 20.4  ni ruzuku ya mishahara, ruzuku ya miradi ya maendeleo ikiwa ni bilioni 2, matumizi mengineyo ikiwa ni milioni 716 na mapato ya ndani yakiwa zaidi ya bilioni 2.4 huku mchango wa jamii ikiwa ni zaidi ya milioni  500.

Akiwasilisha bajeti hiyo katika kikao maalum cha baraza la madiwani, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe , Ally Juma Ally alisema kuwa bajeti ya mwaka 2020/2021 imeongezeka kwa asilimia 24.77 ukilinganisha na bajeti iliyoidhinishwa na bunge ya mwaka 2019/2020 ambayo ilikuwa na kiasi cha zaidi ya bilioni 20.

“Mheshimiwa mwenyekiti ongezeko la bajeti limetokana na kuongezeka kwa makisio ya vyanzo vya mapato  ikiwemo uwepo wa mradi wa tofali, mradi wa ukodishaji wa magari ya kubeba mawe , mchanga na tofali, mradi wa upimaji wa viwanja eneo la Mtwango pamoja na vyanzo vingine vya mapato” alieleza Ally.

Akielezea maeneo ambayo yamepewa kipaumbele katika Nyanja ya uchumi  kwenye bajeti ya mwaka 2020/2021 alisema kuwa ni kuimarisha soko la mbao la Lunguya na kulifanya kuwa la kisasa, upimaji wa viwanja 150 katika Kijiji cha Lunguya kata ya Mtwango pamoja na kuimarisha mradi wa tofali uliopo Njombe Mjini.

Kuhusu miradi iliyopewa kipaumbele katika sekta ya afya Ally alieleza kuwa Halmashauri imepanga kukamilisha ujenzi wa hospitali ya Halmashauri inayojengwa katika kijiji cha Matembwe Kata ya Matembwe, ukamilishaji wa kituo cha afya katika Kata ya Kichiwa, ukamilishaji wa zahanati ya kijiji cha Lima pamoja na ujenzi wa vyoo bora katika vituo vya kutolea huduma za afya.

Aidha, upande wa sekta ya elimu alitaja vipaumbele kuwa ni kuimarisha  miundombinu ya kutolea elimu ikiwemo  ujenzi wa hosteli katika shule za Ikuna na  Manyunyu pamoja na ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za Ikang’asi na Itova.

Upande wa miradi ya kimkakati, Ally alisema kuwa  Halmashauri ya wilaya ya Njombe, imepanga kuendelea kukamilisha andiko la mradi wa ujenzi wa kituo cha biashara, kuandaa maandiko ya uboreshaji wa masoko ya mbao  ya Nyombo na Mtwango pamoja na ujenzi wa hoteli ya kisasa katika eneo la makao makuu ya zamani yaliyopo Njombe Mjini.

Akichangia kuhusu bajeti hiyo mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Njombe, Valentino Hongoli aliwapongeza wataalamu kwa kuandaa bajeti nzuri ambayo itakwenda kutatua changamoto za wananchi.

“Niwapongeze wataalam kwa kuandaa bajeti ambayo ni shirikishi yenye kuongeza mapato na kuboresha miundombinu katika Nyanja tofauti” alisema Hongoli

Halmashauri ya wilaya ya Njombe inajumla ya Kata 12, vijiji 45 pamoja na vitongoji 227.




Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA February 26, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI WA KUANDIKA TAREHE 28-29/12/2020 December 19, 2020
  • TANGAZO MABADILIKO ENEO LA KUFANYIA USAILI December 25, 2020
  • TAARIFA KWA UMMA-TANZIA February 03, 2021
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE YAKOMBA MILIONI 20 MSHINDI WA KWANZA USAFI TANZANIA.

    April 08, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA NJOMBE, MHE.JUMA SWEDA AKIOGEA NA WAFANYAKAZI WA MAKAO MAKUU YA HALMASHAURI

    February 07, 2025
  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAMETEMBELEA NA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    January 30, 2025
  • KATIKA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI YA WILAYA YA NJOMBE(DCC), DC KISSA AUNDA KAMATI MAALUMU KUCHUNGUZA CHANGAMOTO ZA VIWANDA VYA VIWANDA VYA CHAI WILAYA YA NJOMBE

    January 24, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Huduma za Biashara
  • Huduma za Afya
  • Jarida/Gazeti

Viunganishi Linganifu

  • President's Official Website
  • President's Office,Public Service Management and Good Governance
  • President's Office Regional Administration and Local Government
  • National Bureau of Statistics(NBS)
  • Tanzania Information Services-Maelezo
  • Government Portal

Wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

writingMasterThesis

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Mtaa wa Idundilanga,Barabara ya Songea,Karibu na NMB.

    Anuani ya Posta: S.L.P 547 Njombe

    Namba ya Simu: +255 26 2782111

    Simu Kiganjani:

    Barua pepe: ded@njombedc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma Zetu

Haki Miliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Haki zote zimehifadhiwa